Home » » MAKAMU MKUU WA CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI (MOCU) AZINDUA NA KUONGOZA WATUMISHI ZOEZI LA UPIMAJI HOMA YA INI.

MAKAMU MKUU WA CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI (MOCU) AZINDUA NA KUONGOZA WATUMISHI ZOEZI LA UPIMAJI HOMA YA INI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Mosi (MoCU) Prof ,Faustine Bee akizungumza wakati wa uzinduzi wa Upimaji wa Homa ya Ini kwa Watumishi wa Chuo hicho pamoja na Wategemezi wao, zoezi ambalo linafanyika katika kituo cha Afya kilichopo chuoni hapo . 
Baadhi ya Wauguzi wanaohudumu katika kituo hicho fcha Afya pamoja na Watumishi wa Chuo hicho wakifuatilia hotupa ya Uzinduzi wa zoezi la Upimaji wa Homa ya Ini iliyotolewa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU)
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) ,Eustace Ng'weshemi akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa Homa ya Ini katika Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi .
Baadhi ya Watumishi wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi ,wakiwa katika uzinduzi huo.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) Dkt , Eustace Ngw'eshemi akimuonesha Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi ,Prof Faustine Bee namba ya siri itakayotumika wakati wa kupokea majibu baada ya zoezi la upimaji kukamilika.
Mkuu wa kitengo cha Maabara katika Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika (MOCU) Aniseth Malenga akivuta Damu katika mkono wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Prof Faustine Bee alipoongoza zoezi la upimaji wa Homa ya Ini kwa watumishi wa chuo hicho.
Mkuu wa Kitengo cha Maabara katika kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) Aniseth Malenga akivuta Damu katika mkono wa Mmmoja wa watusmihi katika Chuo Kikuu cha Ushirika ,Julieti Bee wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa Homa ya Ini chuoni hapo.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) Dkt , Eustace Ngw'eshemi akizungumza na mmoja wa watumishi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi kabla ya kumfanyia vipimo.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini .

CHUO kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) kimezundua zoezi la upimaji wa Homa ya Ini kwa Watumishi ,Wategemezi wao pamoja na majirani wa cuo hicho ikiwa ni njia ya tahadhari licha ya kutokuwepo ushahidi wa mlipuko wa ugonjwa huo nchini. 

Serikali inatambua umuhimu wa afya bora kwa watumishi wake kwani afya bora ni rasilimali muhimu kwa maendeleo na maenedeleo ya Taifa yataletwa na wananchi pamoja na watumishi wenye Afya na wenye uwezo wa kuzalisha mali na kutoa huduma stahiki kwa umma wa Tanzania. 

Katika kuzingatia sera na miongozo ya Afya ya mwaka 1990 iliyopitiwa mwaka 2007 ,Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MOCU) kama mdau imeanza kutoa huduma ya upimaji wa Ini kupitia Kituo chake cha Afya kilichopo chuoni hapo. 

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) Prof Faustine Bee akatumia zinduzi huo kutoa wito kwa watu wengine waishio nje ya mazingira ya Chuo hicho kutumia kituo hicho pindi wanapohitaji huduma za matibabu. 

Zaidi ya watumishi 456 wanashiriki katika zoezi la Upimaji wa Ini chuoni hapo huku Menejimenti ikiwa katika mazungumzo na Hospitali ya Rufaa ya KCMC ukiona uwezekano wa Wagonjwa wanaohitaji rufaa kwenda moja kwa moja KCMC badala ya kupitia Hosptali ya Mkoa ya Mawenzi kama ilivyo sasa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa