KAMATI YA PAC YAIPONGEZA WIZARA YA AFYA KWA KUBORESHA SEKTA YA AFYA

Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Japhet Hasunga ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Kanda (KCMC) kwa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la huduma za tiba mionzi kwa matibabu ya wagonjwa wa saratani uliofunguliwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.Mhe. Hasunga ametoa pongezi hizo leo baada ya Kamati ya Bunge ya PAC kufanya ziara ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa jengo la huduma za tiba mionzi kwa matibabu ya wagonjwa wa saratani katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda (KCMC) na kupokea taarifa ya ujenzi unaotarajiwa kukamilika Aprili 30, 2025."Kazi ya kamati...

BILIONI SITA KUKAMILISHA UJENZI WA HOSPITALI YA MANISPAA MOSHI, BILIONI 44 VIFAA TIBA

Na WAF - Moshi, Kilimanjaro Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha zaidi ya Bilioni 44 kwa ajili ya ununuzi wa Vifaa Tiba pamoja na Bilioni 1.8 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Manispaa Moshi ambapo Hospitali hiyo ikikamilika itakua imegharimu Shilingi Bilioni Sita.  Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amesema hayo leo Oktoba 6, 2024 baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya Moshi pamoja na ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Kata ya Mabogini ikiwa ni siku ya Tatu ya ziara yake katika Mkoa wa Kilimanjaro. "Rais Dkt. Samia...

ZAIDI YA BILIONI 23 KUTUMIKA KUSAMBAZA UMEME KILIMANJARO VIJIJINI

✔️VIJIJI 506 VIMEUNGANISHWA NA UMEME KATI YA VIJIJI 519 SAWA NA 97.49%Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa kiasi cha Shilingi Bilioni 23.7 ili kuhakikisha miradi yote ya kusambaza umeme vijijini Mkoani Kilimanjaro inakamilika na kuwapatia wananchi maendeleo ya kiuchumi na kijamiiMkurugenzi wa Umeme Vijijini (REA), Mhandisi Jones Olotu amebainisha hayo mbele ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Kiseo Nzowa Julai 29 Mkoani Kilimanjaro wakati wa utambulisho wa Wakandarasi walioshinda tenda ya kusambaza umeme katika vijiji 13 vilivyokuwa vimesalia. "Hadi sasa tumeunganisha umeme katika vijiji 506 kati ya vijiji...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa