Home » » WATOTO SAME WASHINDIA MIWA

WATOTO SAME WASHINDIA MIWA



na Chalila Kibuda
MWENYEKITI wa Baraza la Watoto Kata ya Kirangare, wilayani Same, Christopher Abduel, amesema hali ya lishe kwa wototo katika kata hiyo, si nzuri kwani walazimika kuishi kwa kula miwa.
Abduel alibainsha hayo hivi karibuni wakati wa ziara ya waandishi kuangalia utekelezaji wa mabaraza ya watoto wilayani Same.
Alisema utaratibu wa wanafunzi kupewa chakula shuleni ulidumu kwa miezi kadhaa, kwani baada ya hapo kulikuwa na ukame uliosababisha mazao kukauka hambani, hivyo kuwalazimu watoto kushindia miwa.
Abduel alisema kukosekana kwa chakula cha uhakika katika kata hiyo, ni moja ya sababu za wanafunzi kushindwa kusoma kutokana na kukosa lishe sahihi ya kuweza kufikiria shule.
“Watoto wa Kirangare wamekuwa ndio wazalishaji katika familia hii ni changamoto ya kuacha haki ya msingi ya kusoma na kuingia katika shughuli za uzalishaji mali,” alisema Abduel.
Alisema watoto wanatakiwa kupata chakula chenye virutubisho ambavyo vitawafanya kuwa na akili ya kufanya vizuri, lakini kwa hali ilivyo sasa wanafikiria juu ya kupata chakula na kuacha masomo.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa