Tukio hilo la kutisha lilitokea Desemba 7 mwaka huu, saa 8 mchana
ambapo mtuhumiwa alikuwa kwenye shamba lake akiendelea na shughuli
mbalimbali za kilimo.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kikavu Chini, Swalehe Juma alisema kuwa
baada ya tukio hilo kutokea wananchi walishikwa na hasira na kwenda
nyumbani kwa mtuhumiwa na kuchoma nyumba yake moto baada ya kuwatoroka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alikiri kutokea
kwa tukio hilo na kusema hadi sasa hawajafanikiwa kumkamata mtuhumiwa.
“Taarifa hiyo tunayo ila mpaka sasa hatujaweza kumkamata mtuhumiwa
ila bado Jeshi la Polisi linaendelea na jitihada zake ili sheria ichukue
mkondo wake,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment