Home » » WANAWAKE 12 WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUWAKEKETA WASICHANA 21 SAME KILIMANJARO

WANAWAKE 12 WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUWAKEKETA WASICHANA 21 SAME KILIMANJARO

Wanawake 12 ambao ni wazazi wa wasichana 21 waliofanyiwa ukeketaji wilayani Same, mkoa wa Kilimanjaro, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Same, wakati waliposomewa mashitaka yao kwa mara ya kwanza tangu wakamatwe mwishoni mwa wiki iliyopita.
Watuhumiwa wote wanashitakiwa kwa kosa la Ukatili dhidi ya watoto na kuwasababisha maumivu makali, shitaka ambalo wote wamekana.
Miongoni mwa washitakiwa, mmoja alikabiliwa na mashitaka mawili, moja akiwa mzazi wa mmoja wa wasichana waliokeketwa na pia akiwa ngariba.
Kutokana na mila na desturi ya baadhi ya makabila nchini, ukeketaji unafanyika japo ni kinyume cha sheria, huku watu wanaokamatwa kuhusika na ukeketaji wakichukuliwa hatua za kisheria.
Kama watapatikana na hatia, wanawake hao wanakabiliwa na kifungo kisichopungua miaka mitano jela au kutozwa faini kubwa.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 30 Desemba 2013, wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.
Chanzo;Edwin mushi blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa