Home » » JENGO LA MALIASILI LANUSURIKA KUPIGWA MNADA

JENGO LA MALIASILI LANUSURIKA KUPIGWA MNADA

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Moshi imetoa zuio la kutouzwa jengo la Ushirika wa Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii lililopo chini ya mradi wa shamba la miti la Rongai wilayani Rombo.
Jengo hilo ilikuwa liuzwe kupitia Kampuni ya udalali ya Mariperanto, ili kufidia deni wanalodaiwa wanaushirika hao na mmoja wa wanaushirika, Manase Seleman.
Chimbuko la kuuzwa kwa jengo hilo linatokana na wanaushirika wenzake kukiuka makubaliano ya kumlipa deni lake kupitia makato ya makusanyo ya mapato katika mradi wa basi baada ya kutumia fedha zake kulifanyika matengenezo.
Inadaiwa siku mbili baada ya kulifanyia matengenezo basi hilo na kuingia barabarani mwaka 1987, mwanaushirika huyo ambaye alikuwa ni dereva aligeuziwa kibao na wanaushirika wenzake na kukamatwa na polisi kwa tuhuma za  wizi wa basi hilo.
Manase anadai wanaushirika wenzake walimtungia kesi ya uongo kwa lengo la kumdhulumu haki yake na ndipo alipoamua kufungua kesi Mahakama Kuu mjini Arusha  mwaka 1987 na tangu mwaka huo ameshinda mara nne zikiwamo rufaa tatu.
Akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki, Meneja mradi shamba la miti Rongai, Julius Mkumbo, alisema jengo hilo ni mali ya serikali na si mali ya wanaushirika.
Alisema wafanyakazi hao waliamua kuunda umoja wao kwa lengo la kujiongezea kipato na kulitumia kuendeshea shughuli zao, hivyo mwanaushirika huyo hawezi kulihusisha na madai anayowadai wanaushika wenzake.
Kutokana na hatua ya mahakama kutoa ruhusa ya kuuzwa kwa jengo hilo, meneja huyo alisema wamewasilisha pingamizi mahakamani kupinga kuuzwa kwa jengo hilo.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa