Home » » WAWILI WAFUKIWA MACHIMBONI MOSHI

WAWILI WAFUKIWA MACHIMBONI MOSHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Wawili wafukiwa machimboni MoshiSHUGHULI za uchorongaji miamba katika machimbo ya moramu ya Longoma, Kijiji cha Masaera, Kata ya Kilema Kusini wilayani Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro, zimesitishwa kwa muda usiojulikana baada ya wachimbaji wawili kuangukiwa na kifusi na kufariki dunia.
Tukio hilo limetokea kukiwa na kumbukumbu ya watu saba kupoteza maisha katika machimbo kama hayo ya Pumuani wilayani humo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika kijiji hicho, tukio hilo lililotokea juzi majira ya saa 8 mchana, wakati vijana hao; Adrian Blessing na Shukuru Temu, wanaokadiriwa kuwa na miaka kati ya 18 na 25, walipoingia kwa kificho katika eneo ambalo lilizuiliwa kufanyika shughuli za uchongaji wa tofali.
Diwani wa Kata ya Kilema Kusini, Kawawa Rudega, alisema tayari serikali kupitia kwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Ibrahimu Msengi, aliyekuwepo eneo la tukio juzi, imetangaza kusitisha shughuli za uchimbaji katika machimbo hayo kwa muda usiojulikana.
“Mkuu wa Wilaya alikuwepo hapa jana (juzi), na aliagiza kusitishwa kwa shughuli za uchongaji wa tofali katika eneo hilo na aliwaagiza Mawakala wa Madini (TMAA), Kanda ya Kaskazini kufika katika eneo hili kwa ajili ya kufanya tathmini ya kina kuhusu usalama wa machimbo hayo,” alisema Rudega.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Husiwajali Kidaya, alisema vijana hao walifikwa na mauti baada ya kukaidi amri ya mmoja wa viongozi wa machimbo hayo, ya kuwataka kutoingia baada ya eneo kubwa kuanza kuweka ufa.
“Ni juzi tu Jumamosi, mwenyekiti wa wachimbaji katika machimbo haya alitoa agizo kwa vijana hawa kutoingia humu ndani, kutokana na hili gema lililokatika kuonekana kuwa na ufa, walikaidi na kuingia jana kwa kuibia kwa kujua haikuwa ni siku ya kazi,” alisema Kidaya.
Alisema baada ya kupokea taarifa za tukio hilo, alihamasisha wananchi ambao walifika na kuanza zoezi la uokoaji wakiongozwa na timu nzima ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa