Home » » SELIAN YADHAMIRIA KUWAINUA WAKULIMA WA ZAO LA MAHARAGE

SELIAN YADHAMIRIA KUWAINUA WAKULIMA WA ZAO LA MAHARAGE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

index7Mahmoud Ahmad Siha Kilimanjaro.
………………………………………..
KITUO cha utafiti wa mazao kanda ya kaskazini,SELIANI kimedhamiria kuwainua wakulima wa zao la maharage  kutokana na kuhamasisha wakulima kulima kilimo hicho kwa kutumia mbegu bora za maharage zinazozaa sana ambazo zimefanyiwa utafiti  ambazo zitasambazwa kwa mawakala wa pembejo za kilimo mapema Septemba mwaka huu.
Utafiti huo unatoa msukumo mpya wa kuzalisha zao hilo kwa wingi na hivyo kuinua kipato cha mkulima ambapo atapata mavuno mengi tofauti na aliyokuwa akiyapata kutokana na kutumia mbegu ambazo hazijatafitiwa.
Mratibu, wa mradi huo,Eunice Zakayo,ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akiwaelezea wakulima wa kijiji cha Mlangoni, wilayani Siha,manufaa yatakayotokana na  utekelezaji wa mradi huo wa kilimo cha mazao ya mbegu bora za maharage zilizofanyiwa utafiti na kituo cha kilimo cha Seliani pamoja na mifuko maalumu ya kuhifadhia mazao,PICS.
Alisema ili kuhakikisha mkulima ananufaika na utafiti huo, kituo cha utafiti wa mazao ya kilimo,cha Seliani,kituo hicho  kinatekeleza mradi ambao utaongeza mavuno kwa wakulima wanatumia mbegu bora za zao la maharage ambazo zimefanyiwa utafiti na zinazaa sana .
Eunice ,ambae pia ni afisa kilimo  mtafiti mkuu alisema mradi huo unalenga kuwawezesha wakulima kulima kilimo cha kibiashara ambapo hekari moja ina uwezo wa kuzalisha magunia kati ya 10 hadi 15  tofauti na awali ambapo wakulima walikuwa wakivuna magunia mawili kwa hekari. .
Eunice, amesema utafiti huo wa mbegu bora za maharage unakusudia  kuhamasisha wakulima kupanda mbegu bora za maharage zilizofanyiwa utafiti zinazaa sana hazishambuliwi na wadudu, magonjwa na haziathiriwi na hali ya hewa
Eunice , alisema kuwa mradi huo unaenda sambamba na  matumizi ya mifuko ya PICS ambayo ni maalumu imetengenezwa kwa teknolojia ya kisasa kwa ajili ya kuhifadhia mazao ya maharage kutoka shambani mifuko ambayo inayakinga na kuyalinda maharage yasipekechwe na wadudu baada ya kuvunwa  kwa kipindi cha miaka mitatu na kuendelea .
Alisema mifuko hiyo mipya licha ya kuwa ni mkombozi kwa mkulima pia ni kifaa bora cha kuhifadhia mazao hivyo wakulima hawatakuwa na sababu ya kuendelea kutumi mitungi na magudulia kuhifadhia mazao yao sanjari na matumizi ya dawa za kuulia wadudu wanaopekecha mazao yakiwa ghalani.
 Eunice, alisema mifuko hiyo ya PICS, ambayo itakuwa ikipatikana kwa mawakala wa mbegu na pembejeo za kilimo tu ili kuepuka kuchakachuliwa na wafanyabiashara .
Alisema mradi  unawajali wakulima wa zao la maharage ili wasipate hasara itakayotokana kwa kuhifadhi mazao yao kwa kutumia vifaa duni ambavyo  vinaruhusu wadudu kuingia na kuishi kupekechua maharage na kuwapatia hasara wakulima.
Alisema kuwa lengo la mradi huo ni kumuinua mkulimana ili apate mafanikio na  kila  mtaalamu wa kilimo kwenye eneo husika atakuwa na shamba darasa ili kutoa elimu ya vitendo kwa wakulima kuhusu kilimo cha  mbegu bora za maharage ambzo zimefanyiwa utafiti ili waweze kuongeza mavuno.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa