Home » » WADAU MBALIMBALI WAOMBWA KUJITOKEZA KUWASAIDIA WALEMAVU

WADAU MBALIMBALI WAOMBWA KUJITOKEZA KUWASAIDIA WALEMAVU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Katibu Mkuu akiwa anatoa msaada katika shule ya watoto wenye ulemavu wa akili  na viungo katika shule ya msingi mreyai iliyoko ndani ya wilaya ya rombo.
 Shaka akiwa anapanda MTI katika shule ya watoto wenye ulemavu mreyai rombo
Shaka akiwa na baadhi ya wanafunzi

Na Woinde Shizza, Rombo
Viongozi wa kisiasa, wafanyabiashara, viongozi wa kiserikali na wafanyajazi wametakiwa kuwajali na kuwathamini sana watoto wenye ulemavu na wanaoishi kwenye mazingira magumu kwani wao pia ni binadamu wanao sitahili kupata haki na mahitajj muhimu ya kibinadsmu

Hayo yamebainishwa  leo na kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka wakati alipotembelea shule ya msingi Mreyai iliyopo wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro yenye  huduma ya watoto wenye ulemavu wa viungo na Mtindio wa akili.

Alisema kuwa ni muhimu kuwajali sana watoto wenye ulemavu kwani wakitengenezwa vizuri na kuandaliwa vizuri kwa kupewa elimu watakuwa viongozi wazuri wa baadae. 

Aidha alivitaka vyama Vya siasa vijielekeze kutatua changamoto na ma tatizo ya watoto ambao ni Walemavu na sio kuendeleza Kufanya siasa hata sehemu ambayo haitakiwi siasa.

"Napenda kuviambia vyama vingine vya siasa, sasa hivi uchaguzi umeisha, ni kipindi cha kufanya kazi na kuachana na  mambo ya siasa, sasa hivi ni kipindi cha kufanya kazi na kutatua matatizo ya wananchi " alisema Shaka.

Kwa upande wa Mkuu wa shule ya msingi Mreyai, Nuruel Laizer alisema kuwa shule hiyo inahudumia wanafunzi wenye Mtindio wa akili na wanafunzi ambao ni walemavu wa viungo,amesema kuwa shule hiyo inakabiriwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ukosefu wa chakula cha wanafunzi, ukosefu wa vitanda na mgodoro ya kulalia Wanafunzi ambao ni walemavu ,baiskeli kwa ajili ya watoto ambao ni walemavu wa miguu.

Alisema kuwa Wanafunzi hao wanakaa katika mabweni hapo shuleni, lakini wanaupungufu mkubwa wa vitanda na mgodoro,  kwani vitanda ambavyo wana vitumia wameviazima kutoka kwa watu na mda wowote wenyewe wanaweza kuja kuvichukuwa.

Aliomba serekali pamoja na wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia ili watoto hao waweze kuishi kwa amani na furaha kama watoto wengine."watoto hawa wana wazazi lakini wazazi hao hawana uwezo na ndio maana wamewaleta hapa ili wapate elimu, hivyo tunaomba sana serekali na wadau mbalimbali wajitokeze kutusaidia"alisema laizer

Shule hii ya msingi Mreyai imepata msaada wa chakula, maharage, malindi, sabuni, mafuta, miswaki na kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka aliaidi kusaidia shule hii vitanda Nane na mgodoro kwa ajili ya wanafunzi hawa wenye ulemavu wa viungo pamoja na Mtindio wa ubongo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa