Home » » AZANIA BANK TAWI LA MOSHI YAKABIDHI ZAWADI YA MBUZI KWA WATEJA WAKE NA VITUO VYA KULELEA WATOTO WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU.

AZANIA BANK TAWI LA MOSHI YAKABIDHI ZAWADI YA MBUZI KWA WATEJA WAKE NA VITUO VYA KULELEA WATOTO WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU.

Wafanyakazi wa Benki ya Azania tawi la Moshi ,wakishusha Mbuzi kwa ajili ya kutoa zawadi ya siku kuu ya Idd kwa baadhi ya wateja wake pamoja na makundi yenye mahitaji maalumu.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi ,Hajira Mmambe akimkabidhi zawadi ya Mbuzi mwakilishi wa Mbunge wa jimbo la Moshi mjini Jafary Michael , Bw ,Bashir Seleman wa kampuni ya Zuhad kwa ajili ya siku kuu ya Idd.
Meneja wa Azania Bank  tawi la Moshi,Hajira Mmambe akikabidhi zawadi ya Mbuzi kwa msimamizi wa kituo cha kulea watoto waishio kwenye mazingira magumu cha Qadria kilichopo kata ya mji Mpya,Alhaji Taqdir Haji Amir kama sadaka ya siku kuu ya Idd.
Baadhi ya watoto wa kituo cha  kulelea watoto cha Qadria kilichopo kata ya Mji Mpya.
Meneja wa Azania Bank akikabidhi zawadi ya Mbuzi kwa mteja wa Benki hiyo Aman Idd Mushi kwa ajili ya siku kuu ya Idd.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi,Hajira Mmambe pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo wakikabidhi zawadi ya Mbuzi kwa mwakilishi wa kampuni ya Ibra line ,Bi Mosi Shayo kwa ajili ya siku kuu ya Idd.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi,Hajira Mmambe akizungumza mara baada ya kukabidhi zaadi ya Mbuzi kwa ajili ya siku kuu ya Idd kwa wateja wake pamoja na makundi yenye mahitaji maalumu.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa