Home » » WATANZNIA WAASWA KUPUNGUZA MATUMIZI YA POMBE

WATANZNIA WAASWA KUPUNGUZA MATUMIZI YA POMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WATANZANIA WAASWA KUPUNGUZA POMBE ILI WACHAPE KAZI
Frank Mvungi- MAELEZO
Watanzania wameaswa kupunguza unywaji wa pombe ili waweze kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa viwanda na kulifikisha taifa kwenye uchumi wa kati ifikapo 2020.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Msaidizi  Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Prof. Ayoub Maghimba amesema kuwa ni vyema watu wakapunguza unywaji wa Pombe ili kutumia muda mwingi katika uzalishaji na kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
“Magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni pamoja na  Saratani,magonjwa ya moyo,magonjwa sugu ya njia ya hewa,seli mundu,magonjwa ya akili na dawa za kulevya,magonjwa ya figo,kisukari,ajali, na magonjwa ya macho yasiyo ya kuambukiza” Alisisitiza Prof. Maghimba.
Akifafanua Prof. Maghimba alisema kuwa utafiti uliofanyika ulionyesha asilimia 15.9 ya wananchi wanavuta sigara, asilimia 29.3 wanakunywa pombe, asilimia 97.2 wanakula mbogamboga na matunda chini ya mara tano kwa siku hali inayowaweka katika hatari ya kupata magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Alisema kuwa unywaji wa pombe uliokithiri unasababisha magonjwa kama saratani ambayo inachangia vifo na wastani wa wagonjwa 109 hugundulika na saratani kila siku hapa nchini.
“Magonjwa yasiyo ya kuambukiza au magonjwa sugu ni magonjwa ambayo mtu akiyapata hawezi kuambukiza wengine na ataishi nayo hadi siku ya kufa.”  Alisisitiza Prof.Maghimba.
Magonjwa haya yamekuwa yakiongezeka duniani kote, hasa kwenye nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara,Tanzania ikiwemo. Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yanachangia asilimia 27 ya vifo vyote duniani.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa