Home » » CCM SHANGWE TUPU KILIMANJARO

CCM SHANGWE TUPU KILIMANJARO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 Imeandikwa na Flora Mwakasala, Moshi

Bendera ya CCM
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kilimanjaro kimeendelea kufanya shangwe katika marudio ya uchaguzi mdogo baada ya kuibuka kidedea katika uchaguzi wa wenyeviti wa vijiji na vitongoji.
Katika marudio ya uchaguzi mdogo uliofanyika wiki iliyopita kwenye vijiji vinne, vitongoji 19 na Wajumbe wa Serikali za Vijiji 53, katika Jimbo la Mwanga CCM ilishinda nafasi zote, na juzi iliibuka kidedea kwa kuchukua viti viwili vya Uenyekiti wa Vijiji.
Mkurugenzi wa Uchaguzi katika Jimbo la Moshi Vijijini ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Butamo Ndalahwa alisema vijiji vilivyokuwa vikirudia uchaguzi ni vitatu, vitongoji 12, pamoja na nafasi 14 za Wajumbe wa serikali ya kijiji cha Okaoni.
Ndalahwa alisema katika nafasi ya Wenyeviti wa vijiji CCM ilishinda vijiji viwili ambavyo ni Mande na Mkomilo huku kijiji cha Msae Nganyeni, kikichukuliwa na NCCR-Mageuzi, pia CCM imeshinda vitongoji tisa, Chadema viwili na NCCR-Mageuzi wakiambulia kimoja, wajumbe wa kata CCM ilishinda wajumbe 13, Chadema mjumbe mmoja.
Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Jonathan Mabihya alisema ushindi unaopatikana katika marudio ya uchaguzi mdogo, unaonesha kuwa wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wamerudisha imani yao kwa CCM.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa