Home » » UNCDF YAWEZESHA UFUGAJI SAMAKI KIBIASHARA BWAWA LA KALEMAWE

UNCDF YAWEZESHA UFUGAJI SAMAKI KIBIASHARA BWAWA LA KALEMAWE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Add caption
  Eneo ambalo linaandaliwa kwa ajili ya bwawa la kufugia samaki katika shamba la kufugia samaki la Ruvu lililopo wilayani Bagamayo. Wafanyakazi wa shamba la kufugia samaki la Ruvu wakitega nyavu kwa ajili ya kuonyesha samaki katika moja ya mabwawa kwenye shamba hilo wakati wa ziara hiyo fupi ya mafunzo. Mmoja wa wafanyakazi wa shamba hilo akiwa ameshikilia samaki aina Sato wanaofugwa kwenye shamba hilo. Meneja wa Shamba la Samaki la Ruvu, Khambo Kanthenga (tisheti nyekundu) akitoa maelezo katika chumba maalum cha kutotolea vifaranga vya samaki kwa viongozi mbalimbali wa Serikali wa wilaya ya Same na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) waliokuwa kwenye ziara fupi ya kupata elimu juu ufugaji wa samaki kibiashara katika shamba hilo lililopo wilaya ya Bagamoyo. Mshauri wa Shamba la Samaki la Ruvu, Per Gjoede akitazama mabwawa ya samaki katika shamba la kufugia samaki la Ruvu lililopo wilayani Bagamoyo. Mkurugenzi wa Shamba la Samaki la Ruvu, Daudi Makobole (wa pili kulia) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Staki (kulia) pamoja na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF)-Tanzania, Peter Malika (kushoto), Mshauri wa Shamba la Samaki la Ruvu, Per Gjoede (wa pili kushoto) baada ya kuhitimisha ziara fupi ya mafunzo katika shamba hilo. Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF) nchini, Peter Malika akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Aisha Amour akizungumza wakati ufunguzi wa warsha ya siku mbilli ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Staki. Mkuu wa wilaya ya Same, Rosemary Staki akitoa salamu kwa wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe wakati wa warsha hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Ofisa Mwandamizi anayeshughulikia uwekezaji katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF), Imanuel Muro akisimamia majadiliano kuhusu wa kampuni ya bwawa la Kalemawe lililopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro wakati wa warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji samaki kibiashara katika bwawa hilo iliyoandaliwa na UNCDF na kufanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mkiurugenzi Msaidizi Idara ya Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dr. Charles Mhina akitoa maoni kwenye warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa kijiji cha Misufini kata ya Ngungu wilaya ya Same, Omari Mganga akiwasilisha maoni wakati wa warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa kijiji cha Mgandu kata ya Bendera wilaya ya Same, Merina Mhando akichangia maoni katika warsha ya siku mbili ya wadau wa mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mtaalamu wa Mawasiliano na Ushirikiano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji ya Maendeleo (UNCDF) nchini, Jacqueline Namfua-Mwombela na Mshirika wa Programu UNCDF, Andulile Mwabulambo wakifurahi jambo wakati wa warsha hiyo iliyofanyika wmishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Pichani juu na chini ni washirki wa warsha ya siku mbili ya mradi wa ufugaji wa samaki kibiashara katika bwawa la Kalemawe iliyoandaliwa na UNCDF na kufanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Aisha Amour katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha hiyo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa