Home » » WANANCHI WAMNG’OA MWENYEKITI WA KIJIJI

WANANCHI WAMNG’OA MWENYEKITI WA KIJIJI



na Rodrick Mushi, Hai
WANANCHI wa Kijiji cha Kwa Sadala, wamemng’oa Mwenyekiti wao wa kijiji, Ernest Samwel, baada ya kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye.
Wananchi hao walifikia uamuzi huo katika mkutano mkuu uliofanyika jana baada ya uongozi uliokuwa umetoka wilayani kutaka kuahirisha mkutano huo.
Hali hiyo ilisababisha mzozo na hatimaye wananchi na uongizi Uongozi wa Wilaya kupitia Katibu Tawala Mpotwa walikubaliana kupigwa kwa kura za kutokuwa na imani na mwenyekiti huyo.
Katika kura hizo, 154 zilimkataa mwenyekiti huyo huku kura 124 zikimtaka mwenyekiti huyo aendelee kuwapo madarakani.
Diwani wa Masama Kusini, Issa Kisanga, alisema miongoni mwa tuhuma zilizomuondoa mwenyekiti huyo madarakani ni kuuza maeneo ya wazi kiholela, kuingiza kijiji kwenye mgogoro na kanisa, kutoa lugha chafu kwenye mikutano ya hadhara, pamoja na kutofanya mikutano ya kusoma mapato na matumizi.
Alisema baada ya hatua hiyo kufikiwa kilichobaki ni wananchi kusubiri uongozi wa wilaya kutangaza taratibu za kumpata mwenyekiti wa kijiji wa muda kwa ajili ya kuongoza kijiji hicho huku kukisubiriwa kutangazwa kwa uchaguzi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kijiji hicho aliyevuliwa uongozi, Ernest Samwel alipopewa nafasi ya kujibu tuhuma zinazomkabili, alipinga baadhi ya malalamiko kama ya uuzaji wa maeneo huku akisema malalamiko mengine ni ya kupandikizwa.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa