Home » » Wakwepa kodi kwenye uuzaji,ununuzi viwanja

Wakwepa kodi kwenye uuzaji,ununuzi viwanja

Moshi.Serikali inadaiwa kupoteza mamilioni ya fedha katika mapato ya uuzwaji viwanja kutokana na udanganyifu unaofanywa na wauzaji, pamoja na wanunuzi wa mkoani Kilimanjaro .
Imebainika kuwa viwanja vingi vinavyouzwa ama kununuliwa mkoani hapa havilipiwi kodi.
Mbali na baadhi ya mawakili wasio waaminifu kuandaa mikataba miwili, miwili lakini baadhi ya viwanja vimeuzwa na wamiliki wake kuficha taarifa halisi za thamani ama bei iliyotumika kuuza viwanja hivyo.
Uchunguzi zaidi umebaini kuwa, taarifa za uthamini wa majengo na viwanja hupotoshwa kwa makusudi na baadhi ya wathamini wanaotambulika ili kuwawezesha wauzaji kukwepa kodi.
Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kilimanjaro,Patience Minga alisema mamlaka yake imeandaa utaratibu wa kuwazawadia wananchi watakaofichua mauzo ya aina hiyo.
“Tuna fedha kwa hiyo kama kuna mtu atatuletea taarifa ya aina hiyo atapata kamisheni lakini tumeshaweka utaratibu wa kutoruhusu kuhamisha umiliki kabla kodi haijalipwa,”alisisitiza Minga.
Kwa mujibu wa Minga, hata kama watadanganya kuhusu bei halisi ya mauzo,lakini wanapotaka kuhamisha umiliki TRA itafanya hesabu za kodi kwa kuzingatia bei ya soko na siyo mikataba.

Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa