Home » » JWTZ wapanda Mlima Kilimanjaro siku ya Uhuru

JWTZ wapanda Mlima Kilimanjaro siku ya Uhuru

Marangu.Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali George Waitara, jana amepokea ujumbe wa maofisa wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) na Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii nchini(TTB), Balozi Charles Sanga baada ya kumaliza kupanda Mlima Kilimanjaro, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 52 ya Uhuru.
Maafisa hao wa Jeshi, pamoja na watendaji wa Bodi ya Utalii, walianza kupanda mlima huo, mrefu barani Afrika Desemba 6 mwaka huu na baadhi kufanikiwa kufika kilele cha Uhuru na kusimika Bendera ya Taifa.
Akizungumza wakati wa kupokea ujumbe huo, Waitara ambaye ndiye muasisi wa mpango huo, uliopewa jina la Uhuru Expedition, alisema lengo la mpango huo pia ni kuhamasisha utalii wa ndani.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa