Home » » Watatu kortini kwa kusafirisha mihadarati

Watatu kortini kwa kusafirisha mihadarati

WATUHUMIWA watatu raia wa kigeni wa kusafirisha dawa za kulevya jana wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi na kusomewa mashtaka matatu tofauti.
Watuhumiwa hao ni Grace Teta Gratu(24) Liberaia, Josian Dede Crepy(25) Togo na Julius Nyaoro raia wa Kenya.
Mbele ya Hakimu Mkazi Moshi Simon Kobelo, Mwendesha Mashtaka wakili wa serikali, Janet Sekule, alidai kuwa watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Mwendesha Mashtaka, Patrick Mwita akisaidiana na Sekule, aliieleza mahakama kuwa Josian na Julius katika vipindi viwili tofauti kati ya Novemba na Desemba, walikula njama na kusafirisha dawa za kulevya kinyume na sheria.
Katika kosa la pili, Mwita alieleza kuwa washtakiwa hao wanashtakiwa kwa kosa la kusafirisha kilo 2.2 ya dawa za kulevya aina ya Heroine, zenye thamani ya sh milioni 88.
Kwa upange wa Grace, Mwendesha Mashtaka  alidai kuwa alikamatwa akiwa na kilo 10.5 za Cacaine zenye thamani ya zaidi ya sh milioni 100.
Washtakiwa hao walikana makosa na kesi hiyo itakuja kutajwa tena Desemba 24 mwaka huu.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa