Home » » MUWSA yaanzisha mfumo mpya kuhifadhi taarifa

MUWSA yaanzisha mfumo mpya kuhifadhi taarifa

MAMLAKA  ya Majisafi na Majitaka Moshi (MUWSA)
MAMLAKA ya Majisafi na Majitaka Moshi (MUWSA)

MAMLAKA ya Majisafi na Majitaka Moshi (MUWSA) imeanzisha kitengo cha mfumo wa kijiografia (GIS) kitakachokuwa na jukumu la kukusanya taarifa za wateja wa maji na kuzihifadhi katika mfumo wa kielektroniki ili kuwezesha utoaji wa huduma sahihi.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mchambuzi wa mfumo huo wa mamlaka hiyo, Idd Semkunde, alisema kuanzishwa kwa utaratibu huo ni sehemu ya mipango ya mamlaka hiyo kujiendeleza,  ili kuweza kutoa huduma kwa wateja wake walioko katika mji wa Moshi na maeneo mengine inayohudumia.
Alisema mfumo huo utasaidia kuwatambua wateja wote wa mamlaka pamoja na taarifa zao, ili kuwa karibu pindi panapotokea tatizo katika miundombinu ya mamlaka hiyo pamoja na urahisi wa kupeana taarifa kwa njia ya simu ya mkononi.
Semkunde alisema katika kuhakikisha utaratibu huo unafanikiwa, mamlaka inafanya mawasiliano na serikali za mitaa, ili kuzungumza na wananchi  wao waweze kutoa taarifa sahihi kwa watumishi wa mamlaka watakaopita kukusanya taarifa hizo.
“Huu ni utaratibu mpya kwa MUWSA lakini pia kwa watu wa Moshi na maeneo mengine yanayohudumiwa na Muwsa, tunaomba wananchi watupe ushirikiano pindi maofisa wa mamlaka wanapofika majumbani mwao, kwani mwisho wa zoezi tunachukua namba za simu kwa sababu baadaye wateja wote wanaohudumiwa na Muwsa watakuwa wanapokea taarifa kwa njia ya simu,” alisema Semkunde.
Alisema mfumo wa kielektroniki wa utunzaji taarifa utakapokuwa umeandaliwa vema mamlaka itakuwa kwenye kiwango ambacho mteja hatakuwa na haja ya kupanga foleni kulipia ankara
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa