Home » » Wananchi Mwanga walalamikia operesheni ya polisi

Wananchi Mwanga walalamikia operesheni ya polisi

Moshi. Kamatakamata ya watu wanaoshukiwa kuiba mabomba ya maji nyumbani kwa Waziri mkuu mstaafu, Cleopa Msuya, imeibua malalamiko miongoni mwa wakazi wa Wilaya ya Mwanga.
Mabomba hayo 80, yanadaiwa kuwa na thamani ya Sh2,485,000 na tayari watu sita wamefikishwa mahakamani kwa nyakati tofauti wakihusishwa na tukio hilo.
Takribani watu 30 wamekamatwa na kuhojiwa tangu uchunguzi ulipoanza, baadhi ya watuhumiwa wakiwatuhumu baadhi ya polisi wasiokuwa waaminifu kuomba rushwa ya hadi Sh500,000 ili wawaachie.
Alipoulizwa kuhusu tukio hilo, Mbunge wa Mwanga ambaye pia ni Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe, alisema hata yeye amelifahamu juzi.“Kuna wananchi wengi wakiwa ni vijana wamekuja na kulalamika kuwa kuna operesheni inayowaletea usumbufu mkubwa watu wasiohusika na huo wizi,”alisema mbunge huyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa ni Kilimanjaro, Robert Boaz, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo nyumbani kwa Msuya na kutahadharisha uchunguzi huo usipotoshwe kwa sababu zozote zikiwamo za kisiasa.
“Uchunguzi wowote wa kipolisi unaweza kugusa watu mbalimbali, tusiibue malalamiko yasiyokuwa na ushahidi ili haki isitendeke, uchunguzi ni wa kijinai lazima washukiwa wahojiwe, ”alisema.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa