Hai. Katibu Tarafa wa wilayani hapa, Nsajigwa
Udagile amewataka wanakijiji wa Lerai mkoani Kilimanjaro kusaidia
waliopatwa na maafa yaliyotokea kijijini hapa, yaliyosababishwa na upepo
mkali na kimbunga yaliyoezua darasa moja la Shule ya Msingi Lerai.
Katibu Tarafa huyo amezungumza hayo katika mkutano ulioandaliwa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Lerai,Arpakwa Mamasita.
Amesema ni jukumu na wajibu wa kuchangia maafa
hayo yaliyotokea hivi karibuni na kuleta hasara kijijini hapa. Alisema
bila ushirikiano maendeleo ya wanafunzi yatadumaa.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment