Home »
» AJALI MBAYA YATOKEA MWEKA ,MOSHI VIJIJINI YAHUSISHA VX NA DALADALA
AJALI MBAYA YATOKEA MWEKA ,MOSHI VIJIJINI YAHUSISHA VX NA DALADALA
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Ajali imehusisha gari
ya abiria aina ya hiace inayofanya safari zake kati ya Mweka na moshi
mjini na landcruiser VX iliyokuwa imewabeba wanafunzi wa chuo cha
usimamizi na uhifadhi wa wanyama pori Mweka kilichopo Mweka , Moshi
vijijini.Kwa mujibu wa shuhuda wa ajali hiyobwana Fred Mushi
amesema kuwa gari aina ya landcruiser VX iligonga daladala hiyo iliyo
kuwa imesimama kupakia abiria kwenye kituo kimoja maarufu kwa jina la
Kona. Ajali hiyo imetokea muda wa saa 10.30 jioni ya jana
|
Gari
aina ya landcruiser VX iliyokuwa na wanafunzi toka chuo cha Mweka ikiwa
imezama kwenye mtaro na kuharibika vibaya baada ya ajali hiyo mbaya
iliyotokea jioni ya jana |
|
mashuhuda
walikokuwa eneo la tukio wakilitazama gari aina ya landcuriser
iliyokuwa imezama kwenye mtaro baada ya ajali hiyo iliyotokea jioni jana
na kusababisha majeruhi |
|
daladala
iliyogongwa vibaya na landcuriser ikiwa imeharibika vibaya ubavuni
kiasi cha kutoweza kutembea tena lakini Taarifa za awali hali ya dereva
wake inasemekana kuwa mbaya pia idadi ya majeruhi mpaka tunaenda
mitamboni haijajulikana.tutaendelea kukujuza jinsi taarifa
zitakavyofikia kuhusu hali na idadi Ya majeruhi |
0 comments:
Post a Comment