
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi.
Rai hiyo ilitolewa na Meneja wa Hoteli ya Continental ya jijini Dar es Salaam, Betul Chove, wakati akikabidhi msaada wa Shilingi milioni tatu kwa kikundi cha Kiandiko Group cha mkoani Kilimanjaro.
“Kutoa msaada katika vikundi ni mkakati wa hoteli yetu ambao tulijiwekea, ”alisema Chove na kuongeza: “Ni muhimu tukaungana na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk.
Reginald Mengi, katika kuwasaidia wajasiriamali kwani amekuwa mstari wa mbele katika hili na watu na si kwa sababu ni tajiri hapana, ni moyo aliokuwa nao."
Chove alisema kuna wafanyabiashara wengi nchini lakini hawana moyo wa kujitolea kusaidia wengine wanyonge kama ilivyo kwa Dk. Mengi.
Akipokea msaada huo, Mwenyekiti wa kikundi hicho, Ramadhani Mlawa, aliuhushukuru uongozi wa hoteli hiyo na kutaka wafanyabiashara wengine kuiga mfano huo.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment