Kikosi cha Polisi cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro (Kia), kimewakamata mkazi wa Ilala na raia wa Nigeria, kwa
tuhuma za kukutwa na begi lenye kilo 4.8 za dawa zinazodhaniwa kuwa ni
za kulevya.
Mkuu wa Upelelezi wa Viwanja vya Ndege Tanzania,
Hamad Hamad, alisema watu hao walikamatwa jana saa 9 alfajiri wakisafiri
kwenda Accra, Ghana kupitia Adis Ababa, Ethiopia.
Alisema watuhumiwa walikuwa mbioni kuondaka kwa kutumia ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.
Hamad alisema Mtanzania anayeshikiliwa ana hati ya
kusafiria yenye namba AD266957 na raia wa Nigeria, ana hati ya
kusafiria yenye namba A04331402.
“Hizo dawa zimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili zikachunguzwe na kubaini kuwa ni aina gani,” alisema Hamad.
Hamad alisema watuhumiwa hao walitokea jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Kilimanjaro, tayari kwa safari ya kwenda Accra.
“Huyu raia wa Nigeria, alikuwa anamsindikiza huyu
mwanafunzi wa Chuo cha Bandari Dar es Salaam, wakitokea jijini Dar es
Salaam halafu baadaye yeye abaki aendelee na shughuli zake,” alisema
Hamad.
Hamad alisema watuhumiwa hao wako chini ya ulinzi mkali wa polisi huku upelelezi ukiendelea.
Hivi karibuni Kikosi cha Polisi cha Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kilikamata kilo 3.5 za dawa
za kulevya aina ya heroini zikiwa zimefungwa kwenye vifurushi,
zikipelekwa Monrovia, Liberia.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment