Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya ‘Bongo Fleva’ Nassib Abdul ‘Diamond
Platnumz’, mwishoni mwa wiki alikonga nyoyo za wakazi wa Moshi mkoani
Kilimanjaro, alipotumbuiza katika tamasha la wazi la ‘Good Time ya
Ukweli’ lililoandaliwa na kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola.
Wengine waliopanda jukwaani katika tamasha hilo ni mwanamuziki
maarufu wa hip hop nchini, Joh Makini ‘Mwamba wa Kaskazini’ na Jambo
Squad ambao wanatamba na kibao cha ‘Tukunyema’.
Diamond, aliwapagawisha wakazi wa Moshi alipopanda na kibao chake cha
‘My Number One’ huku kwa upande wa Joh Makini, akikonga nyoyo za
wakazi hao kwa wimbo wake ‘Tatizo ni Bei ya Mkaa’.
Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Masoko wa Coca-Cola
Bonite, Christopher Loiruk, alisema kuwa, ana furaha kwa wakazi wa
Moshi kujitokeza kwa wingi katika tamasha la ‘Good Time ya Ukweli na
Coca-Cola’ na kwamba, lengo la tamasha hilo ni kutoa burudani kwa vijana
na kutoa fursa kufurahi pamoja wakipata viburudisho vya Coca-Cola.
Wakazi wa Mbeya walijimwaga Machi 8 viwanja vya CCM Ilomba na kupata
burudani kutoka kwa Wanaume TMK wanaosifika kwa kuimba na kucheza kwa
nguvu wanapokuwa jukwaani, ambako mamia ya vijana walijitokeza kwa
wingi kupata burudani hiyo.
Mfululizo wa burudani hizo utahitimishwa Machi 23 katika fukwe za
Coco Beach jijini Dar es Salaam, ambako wasanii Diamond, Vannesa Mdee
na wengine wengi watashambulia jukwaa kwa nyakati tofauti kwa lengo la
kutoa burudani ya kukata na shoka kwa vijana.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment