Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
ALIYEKUWA mbunge wa Jimbo la Vunjo, Aloyce Kimaro, ametoa wito kwa
wananchi kujiunga kwenye benki za kijamii vijijini (VICOBA) kama njia
ya kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umaskini.
Kimaro alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati akizungumza na vikundi
vya VICOBA kwenye Kijiji cha Kilindini Wilaya ya Moshi Vijijini ambapo
aliendesha harambee ya kuchangia kikundi hicho na kupatikana sh 660,000
huku yeye akichangia sh 200,000.
Aliwataka wanavikundi hao kutumia fursa wanazozipata kujiletea maendeleo na kuondokana na dhana ya kulalamika.
Alisema kupitia vikundi hivyo wananchi wengi wataweza kuendesha maisha yao vizuri ikiwamo kusomesha watoto shule.
Chanzo:Tanzania daima
0 comments:
Post a Comment