Home » » Kahawa iliyoibwa Burundi yakamatwa Dar

Kahawa iliyoibwa Burundi yakamatwa Dar

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
SHEHENA ya magunia 300 ya kahawa kutoka Burundi iliyoibwa wakati ikisafrishwa kutoka nchini humo kwenda nje ya nchi kupitia Bandari ya Dar es Salaam, imepatikana.
Habari zilizopatikana mwishoni mwa wiki kutoka ndani ya Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) zimedai kuwa kahawa hiyo imepatikana na bodi imetuma maofisa wake jijini Dar es Salaam kwa ajili ya uchunguzi.
Kahawa hiyo ilikuwa ikisafirishwa kwenye lori  aina ya Mercedes Benz lenye namba za usajili A 8564 A na tela lenye namba T 808 BLR liliibwa karibu na ghala lililopo Barabara ya Nelson Mandela jijini humo Januari 6, mwaka huu.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa