Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mahakama imetoa amri ya kukamatwa raia wa Pakistan, Kamran
Ahmed ambaye ni mshtakiwa namba moja katika kesi ya utoroshwaji wa twiga
wanne kwenda Uarabuni.
Hati ya kukamatwa mshtakiwa huyo ilitolewa jana na
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa Kilimanjaro, Simon Kobelo baada mshtakiwa
kushindwa kufika mahakamani jana bila kutoa sababu.
Amri hiyo inafuatia ombi lililotolewa na Wakili wa
Serikali, Evetha Mushi baada ya mshtakiwa huyo kutofika mahakamani kwa
siku ya pili mfululizo.
Wakili huyo aliiomba mahakama itoe amri hiyo ili
mtuhumiwa akamatwe na kufikishwa mahakamani leo, na kama alikuwa ni
mgonjwa awasilishe vyeti kuthibitisha ugonjwa wake.
Evetha alisema kitendo cha Ahmed kutofika
mahakamani bila kutoa sababu zozote, kimeisababishia Serikali hasara
kutokana na mawakili hao kusafiri kutoka Dar es Salaam hadi Moshi.
Hakimu Kobelo alikubaliana na ombi hilo la upande wa mashtaka na kuamuru mshtakiwa kukamatwa.
Mwezi uliopita, kesi hiyo ililazimika kuahirishwa
baada ya mshtakiwa kuugua ghafla muda mfupi kabla ya kesi hiyo,
inayowakabili pia Watanzania watatu, kuanza kusikilizwa.
Watuhimiwa wengine ni Hawa Mang’unyuka, Martin Kimath na Michael Mrutu ambao wote wako nje kwa dhamana.
Wanyama waliotoroshwa walikuwa na thamani ya Sh170.5 milioni na walisafirishwa kwa ndege kubwa ya Jeshi la Qatar.
Ushahidi wa awali mahakamani hapo unaonyesha kuwa
wanyama hao walikamatwa katika maeneo ya Mto wa Mbu, Elboreti na
Engaruka wilayani Monduli.
Chanzo;mwananchi
Chanzo;mwananchi
0 comments:
Post a Comment