Home » » Ndesamburo: Soko la mitumba litarejea Kiborloni

Ndesamburo: Soko la mitumba litarejea Kiborloni

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mbunge wa Moshi Mjini (Chadema), Philemon Ndesamburo amewahakikishia wananchi na wafanyabiashara wa Moshi na vitongoji vyake kwamba soko la mitumba litarejeshwa katika eneo la Kiborloni.
Ndesamburo alisema kurejeshwa kwa soko hilo kutoka eneo la muda la Uwanja wa Kumbukumbu ya Mfalme George (Memorial) ni ahadi ya Chadema waliyoitoa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, alitoa kauli hiyo juzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kiborloni, ambayo ni moja ya ngome za Chadema.
Ndesamburo alisema baada Chadema ya kupata ridhaa ya kuongoza halmashauri, azimio la kwanza walilopitisha ni kurejesha soko hilo lakini mkurugenzi wa wakati huo alikataa kutekeleza azimio hilo.
Katika hatua nyingine, madiwani watatu, Peter Kimaro wa Rau, Dk Charles Mmbando wa Soweto na Ovena Kowero wa viti maalumu, wamesema hawajawahi kutangaza nia ya kuwania nafasi ya Naibu Meya.
Nafasi hiyo imeachwa wazi baada ya aliyekuwa akiishikilia, Vicent Rimoy ambaye pia alikuwa Diwani wa Kiborloni, kufariki dunia.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa