Home » » TAKUKURU YAMBWAGA JAJI JONATHANI KORTIN

TAKUKURU YAMBWAGA JAJI JONATHANI KORTIN

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imeibuka kidedea katika kesi ya madai ya fidia ya Sh700 milioni iliyokuwa imefunguliwa dhidi yake na Jaji mstaafu wa Mahakama Kuu, Peter Jonathan.
Jaji Jonathan ambaye sasa ni wakili wa kujitegemea, alifungua kesi hiyo mwaka 2008 akidai fidia hiyo kwa madai ya kudhalilishwa na Takukuru.
Kiini cha kesi hiyo ni kitendo cha Takukuru kumkamata Jaji huyo Juni 5, mwaka 2007 na kumsweka mahabusu ya Kituo Kikuu cha Polisi mjini hapa.
Maofisa wa Takukuru walilazimika kumkamata Jaji Jonathan baada ya kukaidi wito wa taasisi hiyo uliomtaka kutoa maelezo kuhusiana na uchunguzi wa shauri la kughushi nyaraka.
Jaji Jonathan ndiye aliyeandaa hati zinazoonyesha mtoto wa miaka 15, Onass Edward Kyauka alikuwa ameuza kiwanja cha urithi kwa Sh10 milioni kwa mfanyabiashara wa jijini Dar es Salaam, Edward Eugen Mushi.
Hata hivyo, mtoto huyo ambaye wakati huo alikuwa akisoma kidato cha pili, alikanusha kuwahi kufika mbele ya Jaji Jonathan kusaini nyaraka zozote na kwamba, saini iliyokuwapo katika nyaraka hizo haikuwa yake.
Tuhuma hizo ziliifanya Takukuru ifungue jalada la uchunguzi na Jaji Jonathan aliitwa kuhojiwa lakini alikataa akidai kuwa sheria inamlinda kutotoa siri za mteja wake.
Takukuru ililazimika kumkamata Juni 5, mwaka 2007.
 Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa