Home » » WAUGUZI NHINI WAPEWA SOMO

WAUGUZI NHINI WAPEWA SOMO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WAUGUZI nchini wametakiwa kufahamu kuwa wao ni nguzo muhimu katika sekta ya afya na kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu, ili waweze kukumbukwa na jamii pindi watakapostaafu.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Timoth Wonanji, alipozungumza na Tanzania Daima kuhusu hali ya wauguzi katika halmashauri yake.
Alisema wauguzi wanapaswa kuleta mabadiliko katika sehemu zao za kazi na kutumia nguvu walizonazo kuleta mabadiliko katika sekta hiyo pamoja na kuhakikisha changamoto zinazosababishwa na wauguzi zinaondoka kabisa.
“Unajua muuguzi ni nguzo kubwa katika sekta ya afya na wao ndio watendaji wakubwa ukilinganisha na madaktari, hivyo wanapaswa kuacha kitu ambacho kitakuwa kikikumbukwa kwa kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu,” alisema.
Akijibu swali la tatizo la watumishi, mganga huyo alisema tatizo si watumishi, bali ni utendaji kazi wa watumishi hao na kutoa mfano kuwa unaweza ukawa na watumishi 100, lakini utendaji kazi wao ukawa ni mbovu.
Alieleza kuwa suala la utendaji kazi bora ndiyo linalohitajika na si kubaki kusema kuwa wana tatizo la upungufu wa watendaji katika sekta hiyo na kufafanua kuwa wilaya yake haina tatizo la upungufu wa wauguzi.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa