Home » , » KAMISHNA WA POLISI JAMII NCHINI,MUSA ALI MUSA AFANYA ZIARA WILAYA YA MWANGA

KAMISHNA WA POLISI JAMII NCHINI,MUSA ALI MUSA AFANYA ZIARA WILAYA YA MWANGA


Kamishna wa Polisi Jamii nchini ,CP Musa Ali Musa akitia saini katika kitabu cha wageni wakati wa ziara yake wilayani Mwanga.

Baadhi ya askari Polisi wa kada mbalimbali pamoja na viongozi kijiji cha Kisiwani wakimsikiliza kamishna wa Polisi jamii,Musa Ali Musa alipofanya ziara wilayani Mwanga.
Kamishna wa Polisi Jamii,Musa Ali Musa akiwa ameambatana na kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro SACP ,Robert Boaz wakitembelea maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukagua ujenzi wa kituo kipya cha polisi.
Kamanada wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,SACP Robert Boaz akizungumza na maofisa wa Polisi wa kada mbalimbali katika wilaya ya Mwanga (hawako pichani)kabla ya kumkaribisha kamishna wa Polisi jamii nchini ,CP ,Musa Ali Musa.
Kamishna wa Polisi jamii Nchini,Musa Ali Musa akizungumza na maofisa wa Polisi wa kada mbalimbali katika wilaya ya Mwanga (hawako pichani)
Kamishna wa Polisi nchini Musa Ali Musa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa jeshi hilo pamoja na baadhi ya wananchi katika wilaya ya Mwanga.
Kamishana atembelea kituo kikuu cha Polisi wilaya ya Mwanga.
Kamishna wa Polisi Jamii nchini ,Musa Ali Musa akipokewa na gwaride maalumu lililoandaliwa na askari Polisi kituo cha Mwanga.
Kamishna wa Polisi Jamii nchini ,Musa Ali Musa akitizama eneo ambalo linatazamiwa kujengwa kituo kipya cha Polisi.

Kamishna Musa akiondoka eneo hilo mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika wilaya ya Mwanga.
Na Dixon Busagaga

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa