Home » » TAKUKURU YAOKOA BILIONI 38.9/

TAKUKURU YAOKOA BILIONI 38.9/

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema imeokoa zaidi ya Sh bilioni 38.9 zilizotarajiwa kuingia katika mikono ya wajanja wachache kwa mwaka wa fedha 2013/2014.
Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah alisema fedha hizo zimerejeshwa Hazina kutekeleza shughuli nyingine za maendeleo.
Dk Hoseah alisema kiasi hicho ni ongezeko la Sh bilioni 33.59, ikilinganishwa na fedha zilizookolewa mwaka mmoja uliopita.
Alisema hayo kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa viongozi wa taasisi kutoka mikoa yote nchini, unaofanyika mjini hapa.
Alisema fedha hizo zimeokolewa, kutokana na uchunguzi na operesheni mbalimbali na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo, inayotekelezwa katika mikoa tofauti nchini.
Alisema baadhi ya watendaji walikusudia ziingie katika mifuko yao.
"Tutaendelea kuokoa fedha zinazofujwa na wajanja wachache, vilevile katika kipindi hicho tumefungua kesi 327 zikiwamo tatu kubwa zinazohusu viongozi mbalimbali serikalini, waliojihusisha na vitendo vya rushwa na ukiukwaji wa taratibu," alisema.
Akifungua mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama alitaka taasisi hiyo kujitathmini kwa kazi wanayofanya kama inakidhi mahitaji ya wananchi katika suala zima la kukabili vitendo vya vilivyokithiri sekta ya afya, elimu na miundombinu.
"Natambua kazi kubwa mnayofanya lakini naomba muongeze kasi kupambana na wala rushwa wakubwa ambao wameona kwamba rushwa ni sehemu ya haki yao...hii haiwazuii kuendelea kuwadhibiti wala rushwa wadogo, serikali inathamini mchango wenu," alisema Gama.
Chanzo;Habari Leo 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa