Home » » ‘WANANCHI SAME MASHARIKI WAMEKATA TAMAA’

‘WANANCHI SAME MASHARIKI WAMEKATA TAMAA’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
MWANAHARAKATI na mdau wa maendeleo ya wananchi wa Same Mashariki, Allan Mmanyi ‘Mkombozi’ amesema hali ya maisha ya wakazi wa vijiji vingi vya Same Mashariki inasikitisha kwa kuwa wengi wao wamekata tamaa.
Mkombozi anayefuatilia kwa karibu maisha ya wananchi wa eneo hilo mkoani Kilimanjaro, ameliambia gazeti hili kuwa kila siku watu wa Same Mashariki hushukuru Mungu kwa kusema afadhali ya jana kwani, kilimo kama nguzo kuu ya kiuchumi kwao, kimekuwa hakiwaletei tija yoyote.
“Ni hatari ukifika vijiji vya Vuje, Maore, Ndungu, Bombo, Mvaha na milimani ukawauliza wakulima wanachohitaji utawasikia wakilalamika shida yao ni ukosefu wa soko la uhakika la mazao na uhaba wa pembejeo.
“Hawajui nani atawajibika kuwalipa japo fidia kidogo ya hasara waliyopata. Kwa kweli ni ukatili uliopitiliza ambao watu wa Gonja milimani wanafanyiwa… upande wa elimu, ni shida shule chache, walimu hawatoshi, maabara hakuna huku umbali ukiwa kikwazo kwa wanafunzi wa baadhi ya maeneo," alisema.
Alisema anajipanga kufanya mapinzudi ya kilimo na kwamba ameandaa mpango wa kuwawezesha wana Same Mashariki kuepukana na adha hiyo kwa kubuni njia mbadala za kilimo chenye tija.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa