Home » » MWENYEKITI WA CHADEMA NA MBUNGE WA HAI FREEMAN MBOWE AKABIDHI AMBULANCE MBILI KWA HOSPTALI YA WILAYA YA HAI NA HOSPTALI YA MACHAME.

MWENYEKITI WA CHADEMA NA MBUNGE WA HAI FREEMAN MBOWE AKABIDHI AMBULANCE MBILI KWA HOSPTALI YA WILAYA YA HAI NA HOSPTALI YA MACHAME.


Magari mawili ya kubebea wagonjwa(Ambulance) yaliyotolewa na Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe yakiwasili katika viwanja vya soko la Kuni kwa ajili ya kukabidhiwa kwa viongozi wa hosptali ya wilaya ya Hai pamoja na hosptali ya Machame inayosimamiwa na kanisa la KKKT.
Haya ni maneno yaliyoandikwa katika magari hayo.
Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe akiwa amembeba mtoto mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Kuni na kulakiwa na wananchi katika jimbo hilo.
Magari ya wagonjwa yaliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Hai kwa ajili ya wagonjwa jimboni humo.
Mbunge Mbowe akiwa amembeba moja ya watoto waliofika uwanjani hapo kwa ajili ya kushuhudia msaada wa magari ya wagonjwa yaliyotolewa na mbunge huyo kwa watu wa jimbo la Hai.
Muonekano wa ndani wa magari hayo ya kubebea wagonjwa .
Baadhi ya viongozi mbalimbali waliohudhuria shighuli ya makabidhiano iliyofanyika katika uwanja wa Kuni ,Bomang'ombe wilayani Hai.
Wananchi wakiwa wamezingira magari hayo wakiyatizama kwa karibu.
Mbunge wa jimbo la Hai ,akiuzungumza juu ya msaada huo kwa watu wa jimbo la Hai.
Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe akikabidhi nyaraka mbalimbali za magari hayo kwa Baba Mchungaji Asanterabi Swai ambaye pia ni mkuu wa jimbo kwa niaba ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT).
Mmoja wa viongozi wa Machame Hosptal ,Swai akifurahia msaada wa gari hilo la wagonjwa kwa hosptali yake.
Mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe akikabidhi funguo wa gari kwa mganga mkuu wa wilaya ya Hai,Dkt Paul Chawote ,msada uliotolewa kwa ajili ya hosptali ya wilaya ya Hai.
Watumishi wa hosptali ya wilaya ya Hai,wakiondoka katika viwanja hivyo mara baada ya kukabidhiwa gari hilo.
Wananchi wakifurahia msaada huo.
Baadhi ya wananchi waliofika kushuhudia makabidhiano ya msaada huo wa magari ya kubebea wagonjwa.
Mbunge wa Jimbo la Hai ,Freeeman Mbowe akizungumza na wananchi mara baada ya kukabidhi msaada wa magari mawili ya kubebea wagonjwa.  

KWA HISANI YA HAKI NGOWI BLOG
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa