Home » » VURUGU ZAIBUKA SEKONDARI YA KIGONIGONI.

VURUGU ZAIBUKA SEKONDARI YA KIGONIGONI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
VURUGU kubwa zimetokea katika Shule ya Sekondari Kigonigoni wilayani Mwanga Mkoa wa Kilimanjaro, baina ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita na kusababisha baadhi kushikiliwa na polisi huku wengine wakijihifadhi kwa Mtendaji wa Kata ya Kirongwe.
Vurugu hizo zinadaiwa kuibuka baada ya wanafunzi saba wa kidato cha tano kusimamishwa masomo kwa utovu wa nidhamu. Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaibu Ndemanga alisema vurugu hizo zimetokea juzi saa 12 jioni shuleni hapo na kulazimu askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kutuliza vurugu hizo zilizodumu hadi saa 8 usiku ambako baadhi ya wanafunzi walikimbilia kuomba hifadhi kwa mtendaji kata.
“Baada ya hao wanafunzi saba kusimamishwa masomo walitakiwa kwenda kuwaleta wazazi wao, lakini walikaidi agizo hilo na kubaki shuleni huku wakiwashawishi wenzao kufanya vurugu kama ishara ya kuwaunga mkono,” alieleza mkuu wa wilaya.
Alisema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya inafanya tathmini kujua uwapo kuna uharibifu wa mali sanjari na kutafuta chanzo halisi cha vurugu hizo huku Idara ya Elimu Wilaya hiyo ikizungumza na baadhi ya wanafunzi.
 CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa