Home » » KAYA 350 ZAWEZESHWA KIUCHUMI.

KAYA 350 ZAWEZESHWA KIUCHUMI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MFUKO wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) wilayani Mwanga, Kilimanjaro, umeziokoa zaidi ya kaya 350 za vijiji vya Gongoni-Toloha na Karamba Ndea kwa baa la njaa baada ya miradi yao kuziwezesha kaya hizo kufanya miradi midogo ya kiuchumi na kujinunulia chakula.
Kadhalika kaya hizo zimefanikiwa kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) jambo ambalo awali lilisababisha kutokuwa na uhakika wa kupata matibabu.
Ofisa Ushauri na Ufutiliaji wa Tasaf wilayani Mwanga, Frednand Mazuni, alisema kijiji cha Karamba Ndea chenye takribani kaya 520, kaya 200 kati yake zilikuwa na tatizo kubwa la njaa huku baadhi zikila mlo mmoja kwa siku.
Akizungumzia awamu ya tatu ya Tasaf, wakazi wa kijiji hicho, Palesio Makange alisema asilimia kubwa ya wananchi wanajishughulisha na biashara za aina tofauti ikiwamo sukari na nyanya kutoka Mwanga mjini na kusambaza kijijini hapo na vya jirani.
Awali “Tunaishukuru Tasaf kwani awali wanawake walinyanyasika sana na mfumo dume, sasa wananunua mazao ya chakula kutoka soko moja kwenda jingine, faida inanunua vyakula nyumbani,” alisema.

wali wanawake hawakuwa na sauti katika fedha zilizokuwa zikipatikana kutokana na mifugo kama ng’ombe na mbuzi na kwamba wanaume walikuwa wakitumia fedha za maziwa na hata kuuza mifugo bila kumshirikisha mwanamke,” alisema Makange.
Kwa upande wao, wananchi wa vijiji vya Karamba Ndea, Simu Kizungo na Gogoni Toloha waliomba Tasaf kuwasaidia mradi wa kilimo cha umwagiliaji ili kuondokana na tatizo la njaa linalowakabili.
Baadhi ya wakazi wa vijiji hivyo, Rukaya Ramadhani na Amina Ali walisema hali ya kilimo cha kutegemea mvua hakiaminiki na badala yake wanapata hasara ya mazao yao. Walisema awali mradi huo ulifanyiwa tathmini kwamba ungegharimu Sh milioni 68 lakini haukutekelezeka kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao.
 CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa