Home » » AOMBA WAJAWAZITO, WATOTO KUSAIDIWA

AOMBA WAJAWAZITO, WATOTO KUSAIDIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Imeandikwa na Nakajumo James, Moshi
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadik.
WADAU wa maendeleo wameombwa kuchangia sekta muhimu ikiwamo afya ya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano, kwa kuhakikisha wanapata vifaa tiba katika kuepuka vifo visivyo vya lazima.
Mbunge wa Viti Maalumu mkoani Kilimanjaro, Shally Raymond alisema hayo wakati anakabidhi msaada wa mashuka 60 kwa kituo cha afya kata ya Bomambuzi Manispaa ya Moshi kwa ajili ya wadi ya wanawake wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.
“Msaada huu wa mashuka tumeshirikiana na viongozi wa Manispaa ya Moshi na mkoa lengo likiwa ni kusaidia wodi ya wajawazito na watoto...wanawake wanakabiliwa na changamoto kubwa sana, tunahitaji kuwapatia misaada zaidi,” alisema.
Akiwa amefuatana na baadhi ya viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa kata ya Bomambuzi, Mbunge huyo alisema amekusudia kushiriki kupunguza vifo vya wajawazito na watoto.
Mbunge alikuwa akizungumzia mradi wa kuboresha afya ya uzazi kwa kushirikiana na umoja wa vilabu vya wanahabari nchini (UTPC), Mtandao wa Wadau wa Kuboresha Upatikanaji wa Uzazi wa Mpango (Tanzania Coalition for Access to Contraception –TCAC) na Marie Stopes Tanzania (MST).
Kwa upande wake, Mratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto mkoa wa Kilimanjaro, Fatina Rashid, alisema takwimu za mwaka 2014, zinaonesha Wilaya ya Siha ilikuwa na vifo vitatu kati ya vizazi hai 1,000.
Halmashauri nyingine na idadi ya vifo kwenye mabano kati ya vizazi hai 1,000 ni Hai (3), Moshi Vijijini (1) , Mwanga (4), Rombo (1), Same (2) na Manispaa ya Moshi (14). Mwaka 2015 wilaya ya Siha ilikuwa na vifo 2, Hai vifo vitatu, Moshi Vijijini kimoja, Mwanga vifo viwili, Rombo kifo kimoja, Same kimoja na Manispaa ya Moshi ilikuwa na vifo 23.
CHANZO: HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa