Home » » AGIZO LA NAIBU WAZIRI - KILIMANJARO

AGIZO LA NAIBU WAZIRI - KILIMANJARO





Anitha Jonas – MAELEZO

Kilimanjaro
Serikali ya agiza uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro  kujenga kituo cha kuhifadhi Utamaduni wa wakazi wa Mkoa.  
Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Moshi,Mkoani Kilimajaro na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo  Mhe.Annastazia Wambura alipokuwa katika ziara ya kikazi mkoani hapo kufuatilia uendeshaji wa shughuli za kisekta pamoja na kujadili namna ya kuboresha sekta za Wizara .
Mheshimiwa Naibu Waziri Wambura aliendelea kusema  kuna  kila sababu ya kila kwa kila Mkoa nchini kuwa na kituo cha kiutamaduni ambacho kitahifadhi utamaduni wa wakazi wake pamoja  na kuweka historia ya maeneo mbalimbali ya kiutamaduni.
“Uwepo wa kituo hicho utachangia kuongeza utalii wa kiutamaduni pamoja na kukuza pato la mkoa pale wageni watakapo kuwa wakitembelea vivutio hivyo”,alisema Naibu Waziri Mhe.Annastazia Wambura.
Pamoja na hayo Naibu Waziri huyo alitoa  maelekezo kwa  uongozi  wa mkoa ya kuwataka kuanzisha Kamati  za  Maadili katika ngazi ya Halmashauri na Wilaya zitakazo kuwa zikikagua kazi za filamu za wasanii wa mkoa kwa kuhakikisha maadili yamezingatiwa na kamati hizo zitafanya kazi kwa ushirikiano na Bodi ya Filamu Taifa.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick alipokuwa akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya kisekta kwa Mhe.Naibu Waziri alisema Mkoa unakabiliwa na changamoto ya upungufu wa Maafisa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo lakini tayari suala hilo wameanza kulifanyia kazi kwa lengo la kuongeza tija katika sekta hizo.
“Mkoa huu una vivutio vingi vya kiutamaduni ikiwemo maeneo ya matambiko,eneo alipouwawa mangi Sina wa Kibosho hivyo uhifadhi wa Utamaduni wa maeneo ni suala zuri na jambo hili limekuwa likifanywa na nchi zilizoendelea na umewasaidia kuwa ongezea kipato hivyo suala hili tumelipokea na tutalifanyia kazi”,alisema Bw. Sadick.
Halikadhalika naye Afisa Elimu Mkoa alieleza kuwepo kwa changamoto ya usikivu wa matangazo wa Redio kwa Wilaya ya Same na Wilaya ya Rombo.
Pamoja na hayo Mheshimiwa Naibu waziri alitoa wito kwa watanzania wote kutunza mazingira kwa kuacha kukata miti hovyo pia kuendelea kuhifadhi maeneo yale ya asili ikiwemo  maeneo yanayotumika kwa ajili ya matambiko.

           



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa