Home » » Waandishi wa Habari watakiwa kutokubali kutumika na wanasiasa kwa maslai yao binafsi.

Waandishi wa Habari watakiwa kutokubali kutumika na wanasiasa kwa maslai yao binafsi.



Naibu Waziri wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na watangazaji wa Kituo cha Redio cha New Life kilichopo Wilaya ya Hai leo alipowatembelea kuona uendeshashi wa redio hiyo  (watatu kulia) ni Askofu Dkt.Eliudi Issangya na (watano kushoto) ni Meneja Msaidizi wa Redio hiyo Bi. Leah Jackson.

Anitha Jonas – MAELEZO- Kilimanjaro
Kilimanjaro.

Waandishi wa Habari watakiwa kutokubali kutumika na wanasiasa  kwa maslai yao binafsi.
Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Moshi,Mkoani Kilimanjaro na Mhe.Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo alipotembelea Klabu ya Waandishi wa Habari katika mkoa huo.
“Waandishi nyinyi ndiyo wenye dhamana kubwa ya kulinda amani ya nchi kwa kupitia taarifa wanazozitoa katika vyombo vya habari”,alisema Mheshimiwa Naibu Waziri Wambura.
Kwa upande wa Katibu Mtendaji Klabu ya Wandishi wa Habari Mkoani hapo Bw.Nakajumo James alimuomba Mheshimiwa Naibu waziri kusaidia klabu hiyo kupatiwa hati ya kiwanja chao kilichopo Wilaya ya Hai.
“Kupatikana kwa hati hiyo kutasaidia kukuza kipato cha wanachama kwani tunaweza kupata mikopo itakayosaidia kuongeza miradi ya klabu”,alisema Bw.James.
Aidha,Katibu huyo alitoa ombi kwa Mhe.Naibu Waziri la kuomba atoe wito kwa Watendaji na Wasemaji wa taasisi za serikali kupunguza urasimu katika kutoa habari kwa waandishi kwani waandishi wamekuwa wakikabiliwa na changamoto hiyo.
Halikadhalika ziara hiyo ya kisekta ya Naibu Waziri ilihitimishwa kwa kutembelea  Kituo cha Redio cha New Life FM kilichopo Wilaya ya Hai mkoani hapo kwa leo la kujionea uendeshaji wa sekta ya habari pamoja na usikivu wa matangazo yake.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa