Home » » DIPLOMASIA YAHARAKISHA UKUAJI WA MAENDELEO NCHINI KATIKA MWAKA MMOJA YA JPM MADARAKANI

DIPLOMASIA YAHARAKISHA UKUAJI WA MAENDELEO NCHINI KATIKA MWAKA MMOJA YA JPM MADARAKANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


NA. Immaculate Makilika- MAELEZO

Kwa mujibu wa mtandao wa wikipedia diplomasia ni taratibu zinazoratibu mahusiano katika ngazi ya kimataifa kati ya nchi na nchi au nafasi za kisheria nyingine zenye hadhi ya kimataifa, aidha mtandao huu unaendelea kusema kuwa diplomasia ianaratibu majadiliano baina ya nchi moja na nyingine hasa pale nchi mbili au zaidi zikipigana, diplomasia husaidia kusimamisha vita, sambamba na mazunghumzo yanayohusu masuala ya haki, na amani.

Miaka ya hivi karibuni diplomasia inatumika pia kwa masuala ya biashara, uchumi na utamaduni pale nchi zinazoposaini mikataba fulani ya ushirikiano katika masuala mbalimbali, ambayo  huitwa diplomasi ya uchumi.

Katika kipindi cha mwaka mmoja cha utawala wa Rais wa Awamu ya Tano, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli tumeshuhudia ugeni wa viongozi kutoka mataifa mbalimbali duniani, ni dhahiri kuwa hayo yote yanafanyika ili kuhakikisha diplomasia inatumika katika kuleta ama kuharakisha maendeleo hapa nchini.

Oktoba 23 hadi 30  mwaka huu Mfalme Mohammed wa VI wa Morocco alifanya ziara ya kikazi ya siku nne  nchini, kwa lengo la kukuza uhusiano wa kidiplomasia kati ya Morocco  na Tanzania , ambapo ilisainiwa  mikataba 21 ya ushirikiano baina ya nchi hizo, inayolenga kuboresha sekta  za uchumi na teknolojia.

Mikataba hiyo ni pamoja na makubaliano ya jumla katika ushirikiano wa uchumi, sayansi, ufundi, na utamaduni iliyosainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco, Mheshimiwa Salahddine Mezouar

Mwingine ni ule wa kuanzishwa kwa Jukwaa la Mashauriano ya kisiasa baina ya Wizara ya Mambo ya Nje yaTanzania na Morocco, mkataba wa ushirikiano katika sekta ya gesi, nishati, madini, uvuvi,sayansi ya miamba pamoja na ushirikiano katika usafiri wa anga na kuwasaidia wakulima wadogo nchini kwa kuendeleza soko la mbolea na kilimo kupitia Shirika la Mbolea la Morocco(OCP) na Shirika la Mbolea la Tanzania.

 Kama hiyo haitoshi, ziara hiyo pia ilitia saini mikataba ya  makubaliano ya  mashirika ya Bima ya Tanzania na Morocco, pamoja na  ushirikiano baina ya Bodi ya Utalii Tanzania, Kamisheni ya Utalii Zanzibar na Ofisi ya Utalii ya Taifa  nchini Morocco, ambapo Tanzania inatarajiwa kunufaika zaidi kwa kupata utaalamu hasa katika sekta ya utalii kwa vile nchi ya Morocco imekua ikijipatia pato kwa kiasi kikubwa kutokana na sekta hii.

“Morocco imepiga hatua kubwa kwenye utalii na kwamba mwaka 2015 ilipokea watalii milioni 10.5 na mwakani wanategemea kupokea watalii zaidi ya milioni 14 na kwamba Tanzania imeshasaini  makubaliano kwenye  sekta hiyo kwa lengo la kuendeleza hifadhi za nchi na kuutangaza utalii” anasema Rais Magufuli

Sambamba na hili, mikataba mingine ni kuhusu maeneo maalumu ya uwekezaji (EPZA), uendelezaji na utangazaji wa viwanda, usafirishaji kwenye reli kupitia kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (RAHCO) kwa ajili ya ubia kuendeleza reli ya Mtwara – Mchuchuma/ Liganga, ambapo nchi hizo mbili kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kwenda Rabat, mji mkuu wa nchi hiyo iliyopo kaskazini mwa Afrika.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa