Home » » MADIWANI WA MANISPAA YA MOSHI WATEMBELEA OFISI ZA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA).

MADIWANI WA MANISPAA YA MOSHI WATEMBELEA OFISI ZA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA).

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru akizungumza wakati wa ukaribisho wa Madiwani wa Halmashauri ya manispaa ya Moshi walipotembelea ofisi za mamlaka hiyo.
Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakifuatilia maelezo ya awali ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na  Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) alipokuwa akitoa neno la ukaribisho.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi,Raymond  Mboya akizungumza wakati wa utamburisho wa Madiwani waliotembelea ofisi za MUWSA.
Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Michael Mwandezi aliyeongozana na Madiwani wa Halmashauri hiyo akizungumza wakati wa  ziara ya madiwani katika ofisi za MUWSA.
Baadhi ya Madiwani wakiwa katika kikao cha kupokea taarifa za Mamlaka hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Mipango na Huduma za Biashara Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Tumaini Marandu akitoa taarifa ya Mamlaka hiyo kwa Madiwani waliofanya ziara katika ofsi za MUWSA.
Diwani wa kata ya Miembeni ,Mbonea Mshana akichangia jambo katika taarifa ya Mamlaka hiyo.
Diwani wa kata ya Kilimanjaro,Priscus Tarimo akichangia jambo mara baada ya kusikiliza taarifa ya Mamlaka hiyo katika utoaji wa huduma ya maji safi na maji taka kwa wakazi wa manispaa ya Moshi.
Diwani wa kata ya Mabogini,Emanuel Mzava akichangia jambo katika kikao hicho.
Diwani wa kata ya Njoro ,Jomba Khoi akichangia jambo katika kikao hicho.
Diwani wa viti maalumu ,Mama Kowelo  akichangia katika kikao hicho.
Mkurugenzi ,Joyce Msiru akitoa ufafanuzi juu ya hoja mbalimbali zilizoibuliwa na madiwani katika kikao hicho.
Meneja Ufundi wa MUWSA ,Patrick Kibasa akitoa ufafanuz juu ya hoja zilizohusu masuala ya ufundi .
Kaimu Meneja Fedha wa MUWSA ,Rehema Minja akiteleza jambo katika kikao hicho.
Kaimu Meneja rasilimali watu wa MUWSA,Laurian Kessy akichangia jambo katika kikao hicho.
Mkaguzi wa ndani wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,(MUWSA) Benson Maro akizungumza katika kikao hicho.
Baadhi ya Madiwani wakifuatilia maelezo wakati a mjadla katika kikao hicho.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,(MUWSA) Joyce Msiru akiteta jambo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Michael Mwandezi.(kushoto).
Madiwani wakitembelea chanzo cha maji cha Shiri.
Chanzo cha Maji cha Shiri kilichopo wilaya ya Hai.
Madiwani wakiwa katika chanzo cha maji cha Shiri walipofanya ziara kutembelea vyanzo hicho na kupata maelezo.
Madiwani wakipata maelezo kutoka kwa Meneja Ufundi wa Mamlaka hiyo ,Patrick Kibasa namna maji yanavyotibiwa.
Madiwani wakiwa katika chanzo kipya  cha maji cha Mkashiringi .
Meneja Ufundi wa MUWSA,Patrick Kibasa akitoa maelezo kwa madiwani mara baada ya kutembelea chanzo cha maji cha Njoro ya Goha.
Madiwani wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) mara baada ya kuhitimisha ziara ya kutembea ofisi hizo pamoja na vyanzo vya maji.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini. 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa