Home » » HOSPITALI TPC YAANZA KUTOA MATIBABU

HOSPITALI TPC YAANZA KUTOA MATIBABU

na Dixon Busagaga, Moshi
MENEJIMENTI ya kiwanda cha sukari cha TPC cha wilayani Moshi, imesema hosptali ya kiwanda hicho imeanza kutoa huduma za matibabu ya gharama nafuu kwa wakazi wa vijiji vya jirani vinavyokizunguka.
Ofisa Mtendaji Utawala, Jafary Ally, alisema hayo hivi karibuni wakati wa ziara ya wanahabari kutoka klabu ya waandishi ya Mkoa wa Kagera (KPC) waliotembelea kiwanda hicho kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa.
Alisema mbali na huduma hiyo ambayo kwa sasa wakazi wa zaidi ya vijiji vinne wananufaika nayo, pia hospitali hiyo imeendelea kutoa huduma bure kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho pamoja na wategemezi wao baada ya kuboresha eneo hilo.
“Baada ya kufanya maboresho katika eneo la afya hapa kiwandani, hivi sasa mfanyakazi anatibiwa bure yeye na watoto wake wanne,” alisema Ally.
Chanzo: Tanania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa