Home » » IGP MWEMA AKUMBUKA SHUKA KUMEKUCHA, AKEMEA ASKARI KUTUMIA NGUVU KUBWA, SILAHA ZA MOTO KWA RAIA

IGP MWEMA AKUMBUKA SHUKA KUMEKUCHA, AKEMEA ASKARI KUTUMIA NGUVU KUBWA, SILAHA ZA MOTO KWA RAIA

Na Florah Temba, Moshi-Kilimanjaro Yetu

ASKARI polisi hapa nchini  wametakiwa kufanyakazi kwa   kufuata sheria, maadili  na misingi  ya  polisi nchini ikiwa ni pamoja na kuepuka matumizi ya nguvu na silaha za moto katika  kutekeleza majukumu yao ili kuepuka matukio ya kuua raia.

Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Saidi Mwema aliyasema  hayo wakati akifunga mafunzo  ya uongozi mdogo jeshini katika chuo cha taaluma ya polisi moshi  ambapo alisema suala la ulinzi na usalama katika  nchi  ni jukumu la kila mtanzania pasipo kujali nafasi na cheo alicho nacho .

Alisema polisi wanapaswa kuangalia ulazima na umuhimu wa kutumia nguvu katika utekelezaji wa majukumu yao ikiwa ni pamoja na kufuata sheria na kwamba polisi atakayekwenda kinyume atawajibishwa kwa mujibu wa kanuni na sheria za jeshi hilo.

Alisema uwajibikaji wa polisi na wananchi ni jambo la msingi hususani katika kipindi hichi ambacho jeshi hilo linaupungufu mkubwa wa askari ambapo askari mmoja analazimika kuhudumia wananchi 1300 badala ya wananchi 400 kama inavyopaswa kidunia

Aidha alisema takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 89 ya watanzania hawana ufahamu wa kutosha kuhusiana na suala la ulinzi na usalama na badala yake wanaamini kuwa jukumu la usalama ni la Polisi na viongozi jambo ambalo si sahihi.

“Ulinzi na usalama ni jukumu la kila mmoja  na si la polisi wala viongozi pekee,watanzania wote tuwajibike katika kulinda ulinzi na usalama wa nchi,na katika hili tutafanikiwa kukomesha matukio ya kiuhalifu na kuimarisha amani na utuli” alisema Mwema.

Kwa upande wake kaimu mkuu wa chuo cha taaluma ya polisi Bw.Robert Boaz alisema jumla ya askari  2825 kati ya 2865 wamefanya vizuri mitihanai yao na kupandishwa vyeo wakati 41 wamefeli na kutakiwa kurudia kwa wiki moja na watakao faulu ndio watapandishwa vyeo

Naye kaimu mkuu wa mkoa wa kilimanjaro Bw..Elinas Palanjo alisema  askari wasijivunie vyeo walivyovipata bali  watambue kuwa vyeo hivyo ni majukumu  na wanapaswa kuyatekeleza kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa