Home » » Mtoto aleta kizaazaa, atoweka na bastola ya baba yake

Mtoto aleta kizaazaa, atoweka na bastola ya baba yake

Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro linamhoji mkazi mmoja wa mjini Moshi kufuatia kisa cha mtoto wake kutoweka nyumbani na silaha anayoimiliki kihalali.
Bwana Antony Justine mkazi wa kiboroloni mjini Moshi ambaye ni ni mmilikiki halali wa silaha aina ya bastola yenye nambari  PA 21738 V  anadaiwa kuhifadhi silaha hiyo kizembe kiasi cha kusababisha mtoto wake  kuiba silaha hiyo.
Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Roberty Boaz amesema katika mkutano wake na waandishi wa habari kuwa silaha hiyo ilichukuliwa na mtoto wa familia ya Bwana Antony aitwaye Melkzedeck 23.
Mtoto huyo alichukua silaha hiyo na vifaa vingine kisha kuisalimisha kwa polisi baada ya kutoa shinikizo kuwa asibughudhiwe vinginevyo atajiua kwa kutumia silaha hiyo.
Hata hivyo jeshi la polisi kwa kushirikiana na wasamaria wema limefanikiwa kuioka silaha hiyo kutoka mikononi kwa kijana huyo lakini halikufanikiwa kumkamata kwani aliiacha silaha kichakani na kutokomea kusikojulikana.
Kisa hicho bado kinaumiza vichwa vya maafisa wa polisi na hadi sasa uchunguzi zaidi unaendelea kufanyika kubaini chanzo cha tukio hilo.
Kamanda Boaz amesema jeshi la polisi limetoa onyo kali kwa mmliki wa silaha hiyo bwana Antony kwa uzembe wa kuhifadhi basatola yake huku likitoa mwito kwa wamiliki wengine wa silaha kuwa makini katika utunzaji wake vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa