Home » » Bei ya maji Moshi yapanda

Bei ya maji Moshi yapanda

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji nchini (Ewura), imepandisha bei ya maji katika mji wa Moshi na viunga vyake huku ikitoa masharti kwa Mamlaka ya Maji safi na Maji taka mkoani hapa (Muwsa), kuchimba na kutekeleza miradi mitatu ya uchimbaji wa visima vipya.
Taarifa ya Ewura iliyotolewa na kusainiwa na Mkurugenzi Mkuu, Haruna Masebu, kwenda Muwsa inaonesha mamlaka hiyo imeridhia ongezeko hilo la bei mpya ya maji kutumika kuanzia Agosti mosi mwaka huu.
Kwa mujibu wa agizo hilo la Ewura, ongezeko la bei ya maji safi na ma jitaka kati ya mwaka 2013/2014 linawajumuisha wateja wenye dira katika kundi la majumbani, taasisi, biashara, viwanda, magati na kuosha magari.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ambayo Tanzania Daima imefanikiwa kuiona, mamlaka hiyo imepandisha pia bei ya kumwaga maji taka kwa maboza kutoka sh 10,000 hadi sh13,000 kwa mwaka 2013/2014 .
Katika kundi la wateja wa majumbani wenye dira za maji bei imepanda kutoka sh 412 kwa mita za ujazo hadi kufikia sh 495 kwa mwaka 2013/2014. Wale wanaoosha magari bei imepanda kutoka sh 597 kwa mita hadi sh 715,” Ilieleza taarifa hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Muwsa, Mhandisi Cyprian Luhemeja alithibitisha taarifa za kupanda kwa bei ya maji huku akikiri kuwapo kwa agizo la Ewura la kurekebisha bei ya huduma ya maji kuanzia Agosti mosi mwaka 2013.
Chanzo: Tanzania Daima


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa