Moshi. Watu watatu wamefariki dunia papohapo
baada ya kugongwa na basi la Kampuni ya BM Coach, lililokuwa likitokea
Morogoro kwenda Arusha eneo la Gezaulole, wilayani Hai.
Waliofariki dunia ni mwendesha pikipiki na watembea kwa miguu, waliokuwa pembezoni mwa barabara ya Moshi-Arusha.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz
alithibitisha kuwapo kwa ajali hiyo na kwamba, chanzo ni mwendesha
pikipiki kuingia ghafla barabarani bila kuchukua tahadhari.
“Ni kweli kuna ajali imetokea kwenye saa 11:40
hivi pale Wilaya ya Hai, kuna mwendesha pikipiki aliingia ghafla
barabara kuu… dereva wa basi akajitahidi kumkwepa bila mafanikio,”
alisema.
Boaz alisema baada ya kumgonga mwendesha pikipiki
huyo ambaye alikufa papohapo, basi hilo liliyumba na kwenda kuwagonga
watu wengine watano huku wawili wakifariki papohapo.
Kamanda Boaz, alisema watu watatu waliojeruhiwa
katika ajali hiyo walipelekwa Hospitali ya Rufani ya KCMC kwa matibabu,
hadi tunakwenda mitamboni taarifa ya hali zao ilikuwa haijajulikana.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment