Home » » KESI YA TWIHA YATAJWA JANA

KESI YA TWIHA YATAJWA JANA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WASHITAKIWA wa kesi ya kusafirisha wanyama hai zaidi ya 100 wakiwamo twiga na ndege wa aina mbalimbali kwenda Qatar wanapandishwa mahakamani kwa mara nyingine tena jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi.
Kesi hiyo ambayo inafika mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa, inawakabili washtakiwa wanne akiwamo raia wa Pakistan, Kamran Ahmad, ipo katika hali ya sintofahamu baada ya kuahirishwa mara kadhaa baada ya mshtakiwa huyo kutofikishwa mahakamani hapo bila taarifa yoyote.
Machi 25, mwaka huu kesi hiyo iliahirishwa baada ya mshtakiwa huyo pamoja na wakili wake, Edmund Ngemela, kutofika mahakamani bila taarifa.
Kesi hiyo inayosikilizwa mbele ya Hakimu Simon Kobelo, ipo katika hatua ya ushahidi kwa upande wa Jamhuri, imesimama mara kadhaa baada ya mshtakiwa kutofika mahakamani kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo kuugua.
Machi 24, upande wa Jamhuri uliomba kupewa hati ya kukamatwa mshtakiwa huyo, lakini  haikufanikiwa huku pia wakili wa mshtakiwa huyo, Ngemela naye hakufika mahakamani bila kuwapo kwa taarifa.
Katika kesi hiyo, mawakili wa upande wa Jamuhuri, Evetha Mushi na Steven Mwanasenjele, walidai mshtakiwa huyo anaisababishia Jamhuri hasara kwa kuita mashahidi na kuwarejesha bila kutoa ushahidi.
Katika hatua nyingine upande wa Jamhuri umeiomba mahakama kutoa hati ya kuitwa kwa wadhamini wa mshtakiwa huyo kutokana na mwenendo wa sasa wa mshtakiwa kutokufika mahakamani huku kukikosekana kwa taarifa rasmi.
Baada ya kutajwa jana, kesi hiyo  itasikilizwa kuanzia Mei 6 na 7 mwaka huu, ambapo upande wa Jamhuri utaendelea kuleta mashahidi.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Osaka Traders, Hawa Mang’unyuka, Ofisa Mifugo wa shamba la wanyama, Martin Kimath na Ofisa Usalama wa Kadco, Michael Mrutu.
Washtakiwa wote wanakabiliwa na mashtaka mbalimbali ya uhujumu uchumi ikiwamo la kusafirisha wanyama hai zaidi ya 100 wakiwamo twiga wanne na ndege aina mbalimbali kwenda Doha, Qatar na kuisababishia serikali hasara ya sh milioni 170.5.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa