Home » » HALMASHAURI YAJIKANYAGA

HALMASHAURI YAJIKANYAGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
HALMASHAURI ya Wilaya ya Moshi Vijijini, imekana ahadi yake iliyotoa mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda mwaka 2009, ya kumlipa mkandarasi aliyejenga kituo cha polisi kilichopo Kijiji cha Mkomilo Kaya ya Okaoni.
Uchunguzi uliofanywa ma TanzaniaDaima umebaini kuwa kituo hicho kilijengwa kwa nguvu ya wananchi kwa ushirikiano na jeshi la polisi nchini na tangu kizinduliwe mwaka 2010, na Rais Jakaya Kikwete, mkandarasi huyo hajalipwa zaidi ya sh. milioni 90.
Akizungumza na gazeti hili juzi, Mkurugenzi wa Kampuni ya SAMM Construction, Elikunda Msaki, alikiri kutolipwa fedha alizotumia katika ujenzi huo na kutishia kwenda mahakamani kuomba ridhaa ya makahakama imrejeshee majengo hayo.
Juzi mkurugenzi wa halmshauri hiyo, Fullgence Mponji alikana halmashauri yake kutoa ahadi hiyo huku akidai kuwa mwenye dhamana ya kumlipa mkandarasi huyo ni yule aliyeingia naye mkataba wa ujenzi ambao ni wananchi wa tarafa ya Kibosho.
Halmashauri hiyo iliahidi kubeba gharama za ujenzi wa kituo hicho mbele ya Pinda ambaye aliweka jiwe la msingi la ujenzi wake, ulioasisiwa na wanachi wa tarafa ya Kibosho waishio jijijini Dar es Salaam baada ya kukithiri kwa matukio ya ujambazi wa kutumia silaha ulioambatana na mauaji ya raia.
Wakati mkurugenzi akikana halmashauri yake kutoa ahadi hiyo, mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Morris Makoi aliwaambia waandishi wa habari hivi karibuni kuwa halmashauri yake inao wajibu wa kumlipa mkandarasi huyo na kwamba tayari mwaka jana walimlipa sh. milioni 30 kwa ajili ya kupunguza deni.
Alisema kuwa halmashauri yake ilipanga kuweka fedha kwa ajili ya kumlipa mkandarasi huyo kwenye bajeti yake ya mwaka wa fedha 2013/2014 lakini hadi sasa haijafanya hivyo.
Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa katika mkutano mkuu wa 29 wa ALAT Taifa uliofanyika Mei mwaka jana jijini Arusha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Hawa Ghasia aliiagiza halmashauri hiyo kuweka kwenye bajeti yake deni la mkandarasi huyo.
Kituo hicho chenye hadhi ya daraja B, ujenzi wake umegharimu zaidi ya sh. milioni 300, ambako Jeshi la Polisi nchini lilichangia sh. milioni 70 huku mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kiuto hicho, Cyril Makoi akichangia zadi ya sh. milioni 16 na nguvu ya wanachi ikiwa zaidi ya sh. milioni 100.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa