Home » » MSUYA;MCBL IWE BENKI YA BIASHARA

MSUYA;MCBL IWE BENKI YA BIASHARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Benki ya Wananchi Mwanga (MCBL)WAZIRI Mkuu Mstaafu Cleopa Msuya ameushauri uongozi wa Benki ya Wananchi Mwanga (MCBL) kuibadili kutoka benki ya wananchi na kuwa ya biashara ili ya kupanua wigo na kufungua matawi kwenye mikoa mingine.
Msuya alitoa ushauri huo hivi karibuni alipokuwa akichangia namna ya kuifanya MCBL kukua katika mkutano mkuu wa 14 wa mwaka uliofanyika wilayani Mwanga, Kilimanjaro.
“Ningependa kushauri MCBL ibadilishe utoaji huduma zake kutoka benki ya wananchi na kuwa benki ya biashara… itasaidia kupanua wigo wake na kufungua matawi mikoani,” alisema.
MCBL ilitangaza mafaniko yake kibiashara kwa kupata faida ya sh milioni 68 kwa mwaka wa fedha 2012/2013 licha ya changamoto nyingi zinazoikabili.
Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima jana  Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Abby Ghuhia, alisema faida ya mwaka 2013 imeshuka ikilinganishwa na mwaka 2012 kutokana na gharama za uendeshaji kuongezeka baada ya kufungua vituo vya huduma Moshi Mjini na Same.
Aliongeza kuwa mtaji wa hisa umeongezeka kutoka  sh milioni 555 hadi sh milioni 567 sawa na ongezeko la sh milioni 12.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa