Home » » ONGEZEKO LA WATU LINAHARIBU MAZINGIRA

ONGEZEKO LA WATU LINAHARIBU MAZINGIRA

 Mhifadhi wa Kinapa, Erastus Lufungulo
ONGEZEKO la watu kuzunguka Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (Kinapa), limeathiri mazingira na kutishia kutoweka kwa msitu wa nusu maili.
Hayo yamo kwenye taarifa ya Mhifadhi wa Kinapa, Erastus Lufungulo alipozungumza na waandishi wa habari waliotembelea miradi ya kijamii inayofadhiliwa na hifadhi hiyo chini ya Idara ya ujirani mwema katika sekta ya elimu, afya, maji na mazingira.
Alisema kukithiri kwa uharibifu wa mazingira katika ukanda wa nusu maili kumeathiri mfumo wa ikolojia na maji ambako baadhi ya uharibifu huo ni kusogezwa kwa eneo la ukanda huo.
Kwa mujibu wa Lufungulo, eneo la nusu maili limepungua kutokana kilometa za mraba 88.18 tangu ilipoanzishwa mwaka 1941 hadi kilometa za mraba 51.2 kulingana na mabadiliko ya mipaka yaliyofanyika mwaka 2005.
Athari nyingine ni ongezeko la matukio ya moto katika msitu wa asili kwa upande wa juu yaliyosababisha eneo hilo kuwa vichaka vifupi na kupungua kwa uoto wa asili.
Mhifadhi huyo alisema juhudi zinafanywa kwa ushirikiano na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama aliyepiga marufuku watu kukata miti kwa ajili ya mbao bila kibali kutoka ofisini kwake.
 Chanzo:Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa